Monday, November 22, 2010

VOTE FOR Diamond-URBAN PULSE

Vitalis Maembe entertains (MichuziBlog)

mwenyekiti wa CHADEMA mbeya ajiuzulu nafasi hiyo

Na Francis Godwin
MWENYEKITI wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Mkoa wa Mbeya,Sambwee Shitambala ambaye pia alikuwa mgombea ubunge Jimbo la Mbeya Vijijini amejiuzuru nafasi hiyo kutokana na kutuhumiwa kuwa amehogwa Sh.Milioni 600 na Chama cha Mapinduzi (CCM) na hivyo kusababisha ashindwe kwenye kinyang’anyiro cha ubunge wa jimbo hilo.
Ametangaza uamuzi huo jana wakati akizungumza na waandishi wa habari kuelezea tathimini ya uchaguzi mkuu wa uliofanyika Oktoba 31 mwaka huu mbela ya Katibu wa Chadema Mkoa wa Mbeya,Eddo Makata na Kaimu Mwenyekiti wa Vijana Chadema mkoa,Exavery Mwalembe.

Shitambala alisema amechukua uamuzi wa kujiuzuru nafasi hiyo ya Mwenyekiti wa Chadema mkoa ili kupisha uchunguzi uweze kufanyika ndani ya chama kufuatia tuhuma zambazo zinaelekezwa kwake kwamba kushindwa kuchaguliwa kuwa mbunge wa jimbo la Mbeya Vijijini kumetokana na kuhongwa fedha na CCM.

Alisema shutuma zinazoelekezwa kwake ambazo pia zinatolewa na wanachama wa Chadema na viongozi zimemshushia hadhi mbele ya jamii na utendaji wake wa kazi ya uwakili kama mwanasheria hivyo njia pekee aliyoamua kuchukua ni kujiuzuru nafasi ya Mwenyekiti wa Chadema Mkoa wa Mbeya kwa lengo la kupisha uchunguzi uweze kufanyika kubaini kama kuna ukweli wa tuhuma hizo.
“Maneno yanayozungumzwa kwamba nimehongwa fedha yamepunguza imani kubwa sana kwa wananchi ambapo sasa wamesahau hata mambo mazuri niliyofanya ya kukijenga chama mkoa wa Mbeya,kutokana na hali hiyo nimeona ni bora niachie ngazi na nitabaki kuwa mwanachama wa kawaida ndani ya chama,”alisema Shitambala.

Alisema tangu kumezuka uvumi huo ndani ya chama,amejaribu kumpigia simu Mwenyekiti wa Taifa wa Chadema,Freeman Mbowe, lakini bahati mbaya hapokei simu jambo ambalo linanisikitisha na kutoamini kama ni kweli muda wote anakuwa bize kiasi kwamba ashindwe kupokea simu yangu.

Alisema kinachompa mashaka ni kwanini tuhuma za kuhongwa fedha na CCM zinaelekezwa katika jimbo la Mbeya vijijini wakati yapo majimbo kama Songea, Njombe, Segerea, kilombero, Arumeru, Kiteto, Busanda, Bukoba na Tarime ambayo Chadema ilikuwa na uhakika wa kuibuka na ushindi lakini wagombea wake wameshindwa na hakuna tuhuma kama hizo.

Shitambala alisema kutokana na kuwepo kwa tuhuma hizo zinazoelekezwa kwake tu anaamini kuwa kuna jambo limejificha ndani yake hasa ikizingatia kuwa hii ni mara ya pili kutuhumiwa hivyo ambapo mara ya kwanza ilikuwa wakati wa uchaguzi mdogo wa Jimbo la Mbeya Vijijini uliofanyika mwezi Januria 2008.

Katika uchaguzi huo mdogo Shitamba aliondolewa kugombea ubunge na Tume ya Taifa ya Uchaguzi kwa kukosea mashariti ya kiapo ambapo badala ya kuapa mahakamani aliapa kwa wakili kitu ambacho kinapingana na kanuni za viapo vya uchaguzi na hivyo kukaibuka maneno kwamba alihongwa fedha na CCM ili afanye makosa hayo hasa ikizingatia kuwa ni mwanasheria anayefahamu sheria.
Shitambala alisema kimsingi yapo mambo mengi yaliyosababisha ashindwe kwenye kinyang’anyiro cha ubunge uchaguzi wa mwaka huu ikiwemo jiografia ya jimbo la Mbeya vijijini na pia baadhi ya mawakala wake hususani wa kata ya Inyala ambao walikimbia na hawajulikani waliko hadi sasa.

“Mambo yaliyochangia nijitoe ni kutuhumiwa kwa mara ya pili hivyo nadhani watu wa Mkoa wa Mbeya ni wapenda majungu hivyo hakuna haja ya kuendelea kuwa Mwenyekiti wa Chadema mkoa ,tuhuma ya kwamba sikuweka mawakala siyo za kweli niweka mawakala kila kituo na nikawalipa japo wapo waliokimbia na mpaka leo hii tunaendelea kuwatafuta,”alisema Shitambala.

Alisema wakati umefika kwa wanachama wa Chadema wawe wanajenga imani kwa viomngozi wao kwa kutambue kuwa nguvu ya mgombea wao ikoje kwa mpinzani wake badala ya kuwa wepesi wa kupokea propaganda na wepesi wa kumeza ndoani.

Aliongeza kuwa kwa hali iliyojitokeza Mbeya inawezekana propaganda hii ya kwamba amehongwa fedha ili kuuza jimbo ilienezwa na mtu mmoja tu lakini wanachama wengi wamechukulia kama ni jambo la kweli hali ambayo ni hatari kubwa kwa chama.

Shitambala alisema wana Chadema wafahamu kuwa kamwe hawezi kuuza heshima yake kwa pesa maana yeye si Malaya wa siasa kwani anategemea busara zangu si kwa pesa.

Alisema pamoja na kujiuzuru kwake hana mpango wa kuhamia chama chochote cha siasa na kwamba kama ataamua kuhamia chama kingine cha siasa itakuwa ni maamuzi yake hayatakuwa maamuzi ya kununuliwa.
“Sina wasiwasi na maisha kiasi kwamba mpaka nikubali kununuliwa kirahisi.iwe CCM, TLP au chama chochote cha siasa wakinitaka sitawakubalia nitabaki kuwa mwanachama wa Chadema japo vyama vingi vimekuwa vikinitaka lakini sina mpango wa kwenda chama chochote ikitokea ni maamuzi yangu,”alisema Shitambala.
Hata hivyo kujiuzuru kwa Shitambala kumeelezwa na wachambuzi wa masuala ya kiasia kwamba itakuwa ni pigo jingine kwa Mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi maarufu Mr. Sugu ambaye kimsingi kuchaguliwa kwake kumetokana na msaada wake mkubwa.

Pia uamuzi huo wa Mwenyekiti wa Chadema mkoa ni pigo na athali kwa chama hicho mkoa wa Mbeya kwani katika kipindi cha mwaka huu viongozi wawili wamejiuzuru na kufukuzwa ambapo wa kwanza alikuwa ni Ipyana Seme ambaye aliyekuwa Katibu wa Chadema Wilaya ya Mbeya Vijijini ambaye alifukuzwa na viongozi wa makao makuu ya chama .

Katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu uliomalizika Oktoba 31 mwaka mgombea wa CCM, Mchungaji Luckison Mwanjale aliibuka kidedea wakati nafasi ya pili ilishikiliwa na Sambwee Shitambala wa Chadema

mwenyekiti wa CHADEMA mbeya ajiuzulu nafasi hiyo

Na Francis Godwin
MWENYEKITI wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Mkoa wa Mbeya,Sambwee Shitambala ambaye pia alikuwa mgombea ubunge Jimbo la Mbeya Vijijini amejiuzuru nafasi hiyo kutokana na kutuhumiwa kuwa amehogwa Sh.Milioni 600 na Chama cha Mapinduzi (CCM) na hivyo kusababisha ashindwe kwenye kinyang’anyiro cha ubunge wa jimbo hilo.
Ametangaza uamuzi huo jana wakati akizungumza na waandishi wa habari kuelezea tathimini ya uchaguzi mkuu wa uliofanyika Oktoba 31 mwaka huu mbela ya Katibu wa Chadema Mkoa wa Mbeya,Eddo Makata na Kaimu Mwenyekiti wa Vijana Chadema mkoa,Exavery Mwalembe.

Shitambala alisema amechukua uamuzi wa kujiuzuru nafasi hiyo ya Mwenyekiti wa Chadema mkoa ili kupisha uchunguzi uweze kufanyika ndani ya chama kufuatia tuhuma zambazo zinaelekezwa kwake kwamba kushindwa kuchaguliwa kuwa mbunge wa jimbo la Mbeya Vijijini kumetokana na kuhongwa fedha na CCM.

Alisema shutuma zinazoelekezwa kwake ambazo pia zinatolewa na wanachama wa Chadema na viongozi zimemshushia hadhi mbele ya jamii na utendaji wake wa kazi ya uwakili kama mwanasheria hivyo njia pekee aliyoamua kuchukua ni kujiuzuru nafasi ya Mwenyekiti wa Chadema Mkoa wa Mbeya kwa lengo la kupisha uchunguzi uweze kufanyika kubaini kama kuna ukweli wa tuhuma hizo.
“Maneno yanayozungumzwa kwamba nimehongwa fedha yamepunguza imani kubwa sana kwa wananchi ambapo sasa wamesahau hata mambo mazuri niliyofanya ya kukijenga chama mkoa wa Mbeya,kutokana na hali hiyo nimeona ni bora niachie ngazi na nitabaki kuwa mwanachama wa kawaida ndani ya chama,”alisema Shitambala.

Alisema tangu kumezuka uvumi huo ndani ya chama,amejaribu kumpigia simu Mwenyekiti wa Taifa wa Chadema,Freeman Mbowe, lakini bahati mbaya hapokei simu jambo ambalo linanisikitisha na kutoamini kama ni kweli muda wote anakuwa bize kiasi kwamba ashindwe kupokea simu yangu.

Alisema kinachompa mashaka ni kwanini tuhuma za kuhongwa fedha na CCM zinaelekezwa katika jimbo la Mbeya vijijini wakati yapo majimbo kama Songea, Njombe, Segerea, kilombero, Arumeru, Kiteto, Busanda, Bukoba na Tarime ambayo Chadema ilikuwa na uhakika wa kuibuka na ushindi lakini wagombea wake wameshindwa na hakuna tuhuma kama hizo.

Shitambala alisema kutokana na kuwepo kwa tuhuma hizo zinazoelekezwa kwake tu anaamini kuwa kuna jambo limejificha ndani yake hasa ikizingatia kuwa hii ni mara ya pili kutuhumiwa hivyo ambapo mara ya kwanza ilikuwa wakati wa uchaguzi mdogo wa Jimbo la Mbeya Vijijini uliofanyika mwezi Januria 2008.

Katika uchaguzi huo mdogo Shitamba aliondolewa kugombea ubunge na Tume ya Taifa ya Uchaguzi kwa kukosea mashariti ya kiapo ambapo badala ya kuapa mahakamani aliapa kwa wakili kitu ambacho kinapingana na kanuni za viapo vya uchaguzi na hivyo kukaibuka maneno kwamba alihongwa fedha na CCM ili afanye makosa hayo hasa ikizingatia kuwa ni mwanasheria anayefahamu sheria.
Shitambala alisema kimsingi yapo mambo mengi yaliyosababisha ashindwe kwenye kinyang’anyiro cha ubunge uchaguzi wa mwaka huu ikiwemo jiografia ya jimbo la Mbeya vijijini na pia baadhi ya mawakala wake hususani wa kata ya Inyala ambao walikimbia na hawajulikani waliko hadi sasa.

“Mambo yaliyochangia nijitoe ni kutuhumiwa kwa mara ya pili hivyo nadhani watu wa Mkoa wa Mbeya ni wapenda majungu hivyo hakuna haja ya kuendelea kuwa Mwenyekiti wa Chadema mkoa ,tuhuma ya kwamba sikuweka mawakala siyo za kweli niweka mawakala kila kituo na nikawalipa japo wapo waliokimbia na mpaka leo hii tunaendelea kuwatafuta,”alisema Shitambala.

Alisema wakati umefika kwa wanachama wa Chadema wawe wanajenga imani kwa viomngozi wao kwa kutambue kuwa nguvu ya mgombea wao ikoje kwa mpinzani wake badala ya kuwa wepesi wa kupokea propaganda na wepesi wa kumeza ndoani.

Aliongeza kuwa kwa hali iliyojitokeza Mbeya inawezekana propaganda hii ya kwamba amehongwa fedha ili kuuza jimbo ilienezwa na mtu mmoja tu lakini wanachama wengi wamechukulia kama ni jambo la kweli hali ambayo ni hatari kubwa kwa chama.

Shitambala alisema wana Chadema wafahamu kuwa kamwe hawezi kuuza heshima yake kwa pesa maana yeye si Malaya wa siasa kwani anategemea busara zangu si kwa pesa.

Alisema pamoja na kujiuzuru kwake hana mpango wa kuhamia chama chochote cha siasa na kwamba kama ataamua kuhamia chama kingine cha siasa itakuwa ni maamuzi yake hayatakuwa maamuzi ya kununuliwa.
“Sina wasiwasi na maisha kiasi kwamba mpaka nikubali kununuliwa kirahisi.iwe CCM, TLP au chama chochote cha siasa wakinitaka sitawakubalia nitabaki kuwa mwanachama wa Chadema japo vyama vingi vimekuwa vikinitaka lakini sina mpango wa kwenda chama chochote ikitokea ni maamuzi yangu,”alisema Shitambala.
Hata hivyo kujiuzuru kwa Shitambala kumeelezwa na wachambuzi wa masuala ya kiasia kwamba itakuwa ni pigo jingine kwa Mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi maarufu Mr. Sugu ambaye kimsingi kuchaguliwa kwake kumetokana na msaada wake mkubwa.

Pia uamuzi huo wa Mwenyekiti wa Chadema mkoa ni pigo na athali kwa chama hicho mkoa wa Mbeya kwani katika kipindi cha mwaka huu viongozi wawili wamejiuzuru na kufukuzwa ambapo wa kwanza alikuwa ni Ipyana Seme ambaye aliyekuwa Katibu wa Chadema Wilaya ya Mbeya Vijijini ambaye alifukuzwa na viongozi wa makao makuu ya chama .

Katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu uliomalizika Oktoba 31 mwaka mgombea wa CCM, Mchungaji Luckison Mwanjale aliibuka kidedea wakati nafasi ya pili ilishikiliwa na Sambwee Shitambala wa Chadema

Monday, November 8, 2010

Tahadhari kwa watumiaji wa Internet explorer


Internet Explorer imevamiwa tena,Microsoft wametoa angalizo kuwa kuna uvamizi huu unaoweza kuwapata wale wanaotumia Internet explorer hivyo imewataka watumiaji wake kuwa makini.

Msemaji wa Microsoft amesema kuwa uvamizi huwa unaweza kuwashambulia watumiaji wote wanaotumia matoleo ya 6 na 7.

Katika uvamizi huu,mtumiaji hupokea e mail inayokuwa na link ya tovuti fulani,ukibonyeza hiyo tovuti basi utapelekwa kwenye website yao ambayo wataangalia(test) je unatumia toleo gani la internet explorer,kama watagundua unatumia toleo lenye matatizo ambalo ni la 6 au 7 basi watakupeleka(redirect) kwenye tovuti yao nyingine ambapo wataingiza code kwenye kopyuta yako bila wewe mwenyewe kujijua na kuweza kuitawala kompyuta bila idhini yako.

Kutokana na maelezo kwenye blog ya Microsoft,wanafafanua kuwa hili tatizo linaweza kuathiri hata toleo la 8,ila wamesema toleo la 9 lililopo kwenye majaribio halina matatizo.

Habari njema zinakuja kuwa,ingawa toleo la 8 lipo kwenye utata huu lakini kutokana na udhibiti wake wa kiusalama wa asilia,ni ngumu mtu kuweza kushambuliwa,hivyo kama unatumia toleo la 8 basi upo salama ilihali haujafanya mabadiliko yoyote ya kiufundi tokea uiweke hiyo internet explorer toleo la 8

Hivyo timu ya AfroIT inawashauri wanajamii kutumia toleo jipya la 8 au hata la 9 ili kujihakikishia usaalama zaidi.Ili kudownload toleo jipya la Microsoft tembelea hapa.Pia kuwa makini kwa kutofungua link ammbazo hazina kichwa wala miguu.kwa kufanya hizi utaweza kujiweka katika mazingira ya kiusalama.

Timu ya AfroIT itahakikisha inakuletea habari pindi suluhisho litakapopatikana.

Kwa makala kemkem za ICT tembelea AfroIT leo


Wednesday, November 3, 2010

UCC WON A NATIONAL AWARD!

UCC through its Software Engineering Department has been awarded a National Certificate in ICT for Research in Science and Technology

The Government of Tanzania is now investing heavily in Research and Development for Social and Economic development of the nation. This was stressed by the Minister for Communication Science and Technology at the ceremony to award National Invention and Innovation Certificates. The event was held at Diamond Jubilee Hall on 16th August 2010 where UCC Board Chairman, Prof. Mathew Luhanga received a cheque worth 20,000,000 Tanzanian shillings, a trophy and certificate of recognition for the company

Mrisho Mpoto awabeza wasanii wa kizazi kipya

Msanii mahiri wa mashairi nchini,Mrisho Mpoto ameeleza kile anachoamini kwamba,tasnia ya sanaa na wasanii wa Bongo hawawezi kamwe kupata mafanikio katika ngazi ya kimataifa kutokana na ulimbukeni wa kuiga sanaa za watu wengine, kudharau asili yao na kujipachika usupastaa wa kubumba.

Mpoto aliyasema hayo wakati akiwasilisha mada yake iliyohusu Muziki wa Asili na Mashairi kwenye Jukwaa la Sanaa Jumatatu hii ambapo alisisitiza kwamba,wasanii wa bongo wamekuwa ni wa kulalama na kulia njaa kutokana na kazi wanazozalisha kushindwa kabisa kupata mvuto wa kimataifa na kushindana kwani zimekuwa kwa asilimia kubwa zikifanana na tamaduni za nje hivyo kukosa jipya.

Akijitolea mfano yeye mwenyewe Mpoto alisema kwamba, ameweza kukaa chini na kubuni sanaa ya asili ya Tanzania ambapo amekuwa akighani mashairi na kuyaweka kwenye mdundo wa muziki na hivyo kupendwa na idadi kubwa ya watanzania na kupenya kimataifa hivyo kumfanya kupata mialiko na fursa nyingi za fedha ambazo zimekuwa zikimpatia mafanikio makubwa.

Kwake yeye Mpoto anaamini kwamba, Sanaa ya Tanzania na wasanii wake hawaonekani kugundua siri ya kufanya kazi za sanaa zenye asili yao na badala yake wamekuwa makasuku wa kujifananisha na kuishi maisha kama ya Ulaya na Marekani huku kazi zao zikifanana kila kitu na hizo za nje hali ambayo imeifanya sanaa kupwaya na wasanii wenyewe kuishi maisha ya njaa.

Aliongeza kwamba, ni ngumu kupata msanii wa bongo anayefanya sanaa peke yake kwani mara nyingi lazima wachanganye na shughuli zingine ili kupata kipato kutokana na kazi zao kutowalipa.Katika hili Mpoto anaamini kwa kiasi kikubwa limesababishwa na wasanii wenyewe kukosa ubunifu, kuiga kila kitu kutoka nje, kulewa sifa za mapema, kukumbatia sanaa zisizo za asili yao na kujipachika usupastaa wa kubumba.

“Nimekuwa nikipata mialiko mingi nje ya nchi,siku chache zijazo nitaenda Denmark,Finland,Ufaransa, na Uholanzi.Si kwa kuwa napendwa sana bali ni aina ya sanaa ninayofanya ina asili yangu ya Tanzania na inanitambulisha kila ninakokwenda.Waache wasanii wengine wavae nguo chini ya makalio yao au hata watembee uchi mimi nitabaki na magunia yangu.Hili ndilo naamini litaweza kunipa mafanikio na ninayapata” alisisitiza Mpoto.

Mpoto ambaye kwa sasa ni msanii pekee aliyepata mafanikio makubwa kutokana na kupata mikataba mingi ya matangazo, mauzo ya kazi zake na mialiko ya kimataifa kutokana na kukumbatia sanaa ya asili aliwashauri wasanii wa bongo kuacha kunakiri (kukopi) sanaa za nje na badala yake wakune vichwa katika kubeba sanaa ya asili ambayo hapana shaka itawatambulisha kimataifa na kuwapa mikataba minono ya ndani na ya nje.

Mpoto aliyekuwa ameambatana na muimbaji wake wa Mjomba Band,Ismail alisema kwamba, inatia aibu na kinyaa unapoangalia sanaa za bongo kwani zinaonekana kuandaliwa na watu wenye njaa, wanaosaka fedha za fastafasta kuliko kujali nini wanapeleka sokoni hali ambayo imekuwa ikiwafanya wasanii wa Tanzania waonekane ni wa hovyohovyo, wa kudharaulika na wasio na mkakati wa kufikia mafanikio ya kisanaa.

“Kuna watu wamefanya sanaa miaka nenda miaka rudi lakini hawapigi hatua.Wamekuwa ni watu wa kulalamika bila kuzingatia ni kwa kiwango gani sanaa zao zina ubunifu na kubeba asili na utambulisho wao.Ndugu zangu tusipozingatia haya mafaniko tutayasikia tu na tutakuwa watu wa kuganga njaa na kupiga mizinga ya vocha” alimalizia Mpoto.

ajimbo yaliyokwishatwaliwa na Upinzani

1.Musoma mjini - Vincent Nyerere- CHADEMA
2.Iringa mjini - Mch. Peter Msigwa- CHADEMA
3.Lindi mjini - Salum Halfani Barwani- CUF
4.Arusha mjini- Godbless Lema - CHADEMA
5.Mwanza Nyamagana- Hezekiah Wenje - CHADEMA
6.Moshi Mjini- Philemon Ndesamburo - CHADEMA
7.Maswa Magharibi- John Shibuda- CHADEMA
8.Maswa Mashariki- Silverster Kasulumbayi- CHADEMA
9.Ukerewe - Salvatory Naluyege- CHADEMA
10.Biharamulo - Dr. Mbasa - CHADEMA
11.Ilemela - Haines Samson- CHADEMA
12.Meatu- Meshack Opulukwa- CHADEMA
13.Kigoma Kaskazini- Zitto Kabwe- CHADEMA
14.Mbeya mjini - Joseph Mbilinyi - CHADEMA
15.Hai Kilimanjaro- Freeman Mbowe - CHADEMA
16.Vunjo - Augustino Lyatonga - TLP
17. Kasulu vijijini - Zaituni Buyogera - NCCR Mageuzi
18. Kasulu Mjini - Michael John - NCCR Mageuzi
19. Mbulu -Mustafa Akonay - CHADEMA
20. Ubungo - John Mnyika - CHADEMA
21. Kawe - Halima Mdee - CHADEMA

Uchaguzi ulikuwa Huru na wa Amani

WAANGALIZI wa Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu uliofanyika Oktoba 31,kutoka Jumuiya ya Ulaya ( EU EOM) na Umoja wa Afrika wamesema kuwa uchaguzi huo ulikuwa wa huru na haki, utulivu na amani.

Waangalizi hao walitoa kauli hizo kwa nyakati tofauti wakati walipofanya mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana(leo) kuhusu taarifa ya awali ya uchaguzi huo.

Akizungumza na waandishi wa habari Mwangalizi Mkuu wa EU EOM, David Martin alisema uchaguzi huo ambao ni wa nne kufanyika nchini tangu mfumo wa vyama vingi kuanzishwa Tanzania, hadi sasa kwa ujumla umefanyika kwa amani na mpangilio mzuri.

“ Siku ya Uchaguzi Mkuu ilijitokeza kwa utulivu mkubwa na kwa ujuml a waangalizi wa uchaguzi wa Ujumbe Maaalumu wa Jumuiya ya Ulaya(EU EOM) ulikadria mchakato mzima wa uchaguzi huo kuwa ama ulikuwa ‘mzuri’ au ‘ kuridhisha’ katika asilimia 95 ya vituo vyote vya kupigia kura walivyovitembelea upande wa Tanzania Bara na upande wa Zanzibar,” alisema Martin.

Aliongeza kuwa kwa ujumla taratibu muhimu katika vituo vya kupigia kura zilitumwa kwa ulinganifu kwa kila kituo cha kupigia kura nchini kote, licha kuwepo mapungufu machache.

Martin alisema Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) na Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) zilisimamia chaguzi kwa namna ya kitaalamu, hivyo kwa sehemu kubwa ziliwapatia watu watu wote haki ya kupiga kura.

Aliongeza kuwa ujumbe huo utabakia nchini kuzidi kufuatilia kwa karibu zaidi zoezi la kuhesabu matokeo ya uchaguzi, utangazaji wa matokeo na matukio yoyote yatakayojitokeza baada ya uchaguzi.

“Taarifa hii ni ya awali .Taarifa ya kina ya mwisho itatolewa baina ya miezi miwili na miezi mitatu baada ya mchakato mzima wa uchaguzi kukamilika,” alisema.

Kwa upande wake Kiongozi wa waangalizi hao, kutoka AU, Rais wa zamani wa Jamhuri ya Sierra Leone, Dk. Ahmad Tejan Kabbah alisema uchaguzi huo umefanyika wa amani na umefanyika kwa mujibu wa sheria za uchaguzi wa Tanzania .

Aliongeza kuwa umefanyika kwa kuzingatia Azimia la Durban Demorasia katika Chaguzi za Afrika la Julai mwaka 2002.

“ Waangalizi wa Umoja wa Afrika wamesema uchaguzi umefanyika kwa huru, haki , uwazi na uadilifu(Credible) .

Naye Katibu Mtendaji wa International Conference of the Great Lakes Region (ICGLR) Balozi Liberata Mulamula amesema wiki hii kwamba wameridhishwa na mchakato mzima wa uchaguzi mkuu Tanzania na kwamba ukiondoa matatizo madogo madogo yaliyojitokeza sehemu mbili tatu, ulikuwa huru na wa haki.

Balozi Mulamula amesema uchaguzi wa Tanzania ni mfano wa kuigwa kwa nchi wanachama wa ICGLR ambao wengi watakuwa na uchaguzi katika kipindi hiki. Ameisifu serikali ya Tanzania kwa juhudi zake za kuhakikisha kila kitu kinaenda sawa na kuruhusu kila mwananchi aliejiandikisha kupiga kura bila wasiwasi.

Waangalizi hao ,waliwapongeza wananchi wa Tanzania, Vyama vya Siasa, wagombea , NEC, ZEC na vyombo vya usalama kwa kuwezesha uchaguzi huo ufanyike kwa amani na kuwashauri wagombea kukubali matokeo yanayotangazwa na NEC.