Friday, December 17, 2010

DADA ZETU CHAMBO CHA KUWAPATIA URAIA WAGENI

Kutoka Michuzi Blog
Jana nilipata sijui niite bahati au balaa? Call it eye opener. Nilikwenda kweye msiba huko Mbezi ya Kimara. Katika huo msiba, dada yetu (soma mtanzania) alifariki na “mumewe” ni mtu wa Afrika Magharibi, almaarufu kwa kucheza sinema zenye kuvuta hisia za watu wengi.

Idadi kubwa sana ya raia wa nchi hiyo katika huo msiba ilinifanya nijiulize maswali kadha wa kadha. Wanafanya nini wote hao nchini? Wana vibali vya kuishi nchini kihalali? Si vema ku judge mtu kwa sura yake au alivyo ila kwa tathmini ya haraka kuhusu raia hao wa kigeni, wengi wao niwanalekea ni misheni town.

Raia wengi wa kigeni wanaotaka kuishi nchini wanakimbilia kuwaghilibu dada zetu wawaoe na kuwazalisha ili wapate uhalali wa kukaa bila ya kubugudhiwa. Na dada zetu katika harakati za “to make the ends meet” wanaingia katika mitego hii bila ya kujijua.

Akina kaka nao kwa mbalii wanakuja katika huu mtego. Akishampata mke wa kigeni (wakenya wanaongoza), utitiri wa ndugu wanakuja kwa shem!.Halafu? Malizia sehemu ya mwisho waraka huu

Mlango mwingine usiotamkwa sana unaotumiwa kuwaingiza wageni ni kwa kupitia taasisi za kidini. Kuna makanisa mpaka wafagizi wametoka nje. Watumishi wa Mungu wanaokwenda kupata neno la Mungu katika makanisa hayo wafumbue macho na kuhoji uhalali wa kuleta wafanyakazi toka nje! Tena wahubiri ndo wamechachamaa na kufagilia inter marriages eti kuwa zinaleta maendeleo! (Commercialization of religions)

Sina maana ya ubaguzi ila kama ni kuja nchini waje kwa kufuata taratibu zinazotakiwa na muda wao ukiisha waondoke pasi na hodi. Wamejazana huko kariakoo, Kinondoni na kwenye viwanda, magereji na magodown. Jamani mpaka masokoni nako tunahitaji “maexpatriate”?

Mamlaka husika kwa maana ya vyombo vya uhamiaji na vinavyohusika na usalama wa raia, umefika wakati muafaka wa kuamka usingizini na kutuepusha na balaa linalokuja siku za usoni.

Napata maono ya kuwa inabidi hawa raia waliooa dada/kaka zetu wafuatiliwe kwa kina. Ndoa hizi huwa zinaishia vipi? Kwa divorce? Kwa vifo? Na akina nani wanakufa? Sisi au wao? Hatima ya watoto inaishiaje? Wanatelekezwa au wanachukuliwa/toroshwa kwenda “kwao”?

No comments: