Tuesday, January 25, 2011

Wanafunzi wa Internet TR3 saa 7 mchana

Nimependa hizo nywele zake jamani
Hata haka kasweta nako kanavutia
Mzee wetu ametulia ile mbaya, hii ndio raha ya Computer bwana!!!
Huyu nae macho mbele kwenye projector, safi sana!!
Hapa macho kwemye screen yake, pozi lake lapendeza pia!
Makamanda wangu hawa hapa. Raha hadi jamaa kulia analala, ahahaaa tehe tehe tehe!
Pozi adimu sana!
Mara style ikabadilika! Duh!
Tabasam poa kichizi, Nywele na blauzi yake zimemtoa chicha kikweli!!
Hili ni pozi la kutafakari!!
Kama anataka kucheka vile!!
Mkao wa kupiga picha! Huyu je unamjua?

Dada wa mtandio akifanya vitu vyake, mwenyewe utampenda!

Wednesday, January 19, 2011

Upinde wa mvua leo jioni hapa Arusha

Je upinde wa mvua ni dalili ya mvua kuanza au kuisha? Wadau mnasemaje?

Wanafunzi wangu wa Internet TR3 saa 11 jioni!



Jamaa anaingiza data katika computer, katulia ile mbaya!!

Huyu je unamjua?

Huyu ni Mtaalam wa Internet akifanya vitu vyake

Thursday, January 6, 2011

VIONGOZI WA CHADEMA WASHIKILIWA NA POLISI ARUSHA

Kwa Hisani ya Michuzi Blog
MWENYEKITI WA CHADEMA NA MBUNGE WA HAI MH. FREEMAN MBOWE NI MIONGONI MWA VIONGOZI KADHAA WA CHAMA HICHO AMBAO WAKO MIKONONI MWA POLISI JIJINI ARUSHA DAKIKA HII, BAADA YA KUTIWA MBARONI KWA KILE KILICHOONEKANA KUWA MAANDAMANO BATILI.


TIMU YA GLOBU YA JAMII AMBAYO IKO ENEO LA TUKIO LIMEWATAJA VIONGOZI WENGINE WALIO KOROKORONI KUWA NI MBUNGE WA ARUSHA MJINI MH. GODBLESS LEMA, MBUNGE WA ROMBO MH. JOSEPH SELASINI NA WANACHAMA WENGINE KADHAA WA CHADEMA.


HABARI ZINASEMA POLISI WALITAWANYA MAANDAMANO HAYO YALIPOKARIBIA OFISI ZA TAKUKURU NA KWAMBA BAADA YA VUTA NIKUVUTE, MH. MBOWE NA WENZIE WAKAKAMATWA NA KUTUPWA RUMANDE.


AIDHA HABARI ZINADATISHA KWAMBA JIJI LA ARUSHA LINARINDIMA KWA MPAMBANO WA KUKIMBIZANA WA POLISI NA MAKUNDI YA WATU WANAODAIWA KUTAKA KWENDA KITUO CHA POLISI KUWATOA WALIOKAMATWA KWA NGUVU.
--------------------------------


Mh. Freeman Mbowe akizungumza na Tanzania Daima kutoka Arusha jana jioni alisema maandamano hayo yatakayohitimishwa na mkutano mkubwa wa hadhara, ajenda yake kuu ni kupinga hatua ya serikali kuvunja sheria kwa makusudi na kukipa Chama cha Mapinduzi (CCM) ushindi ulio kinyume cha sheria katika uchaguzi wa umeya uliofanyika hivi karibuni.


Mbowe akizungumza na Tanzania Daima kutoka jijini Arusha jana jioni alisema CHADEMA itaanza rasmi kuitumia nguvu ya umma kupinga kile alichokiita "uhuni uliofanywa na CCM na serikali yake kujipa ushindi wa lazima katika uchaguzi wa umeya kinyume na matakwa ya sheria halali za nchi.


"Mwanza hakujafanyika uchaguzi kwa sababu ya dhuluma, Kigoma na Arusha uchaguzi ulikuwa batili kabisa. Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za mitaa (TAMISEMI) tumemsihi sana aingilie kati lakini ameendelea kushirikiana na chama chake (CCM) kuinyima CHADEMA haki ya kuongoza. Tunakwenda kulaani kwa nguvu zote uchakachuaji wa maamuzi ya wananchi" alisema Mbowe