Friday, May 4, 2012

AJALI YA BASI LA NBS MKOANI TABORA

Basi la abiria la kampuni ya NBS lenye nambari za usajiri T978ATM aina ya Scania, limepata ajali mbaya maeneo ya Jineri kilomita kadhaa kabla ya kufika kwenye mji wa Igunga Mjini Mkoani Tabora na kusababisha vifo vya watu saba papo hapo.Waliopoteza Maisha ni wanaume watatu na wanawake watatu pamoja na mtoto mmoja wa kiume ambao wote majina yao hayakuweza patikana mara moja. Basi hilo lilikuwa linatokea mkoani Tabora kuelekea Jijini Arusha.


No comments: