CHELSEA Tanzania leo imewatangaza wasanii watakaopamba sherehe za
ubingwa zitakazofanyika kwenye ukumbi wa Msasani Beach Club Jumapili
hii. Mbali na michezo itakayozikutanisha Chelsea Tz,Arsenal Tz na
Manchester Tz pia kutakuwa na burudani mbalimbali wakiwemo Mr.Nice,Sweet
Sunday,Muumin Mwinyjuma,Charlesa Baba,Shilole atakayesindikizwa na
Irene Uwoya na Akudo Impact. Kiingilio kitakuwa shilingi elfu 10 kwa
wakubwa na watoto shilingi elfu 1. Sherehe hizo zitaanza tokea saa 4
asubuhi kwa soka la ufukweni.
Sherehe hizo ni mwanzo tu wa mambo mengi makubwa yatakayofuata baada ya
usajili wa Taasisi itakayotambulika pia makao makuu huko London.
No comments:
Post a Comment