Monday, June 11, 2012

SHUKRANI ZANGU KWENU!-BAADA YA MSIBA

Jumatano June 6, 2012 saa 7:32 mchana KAKA yangu mzaliwa wa kwanza aitwaye ABRAHAM JOHN MLAULE (Kulia mwenye tai na miwani) alifariki dunia katika hospitali ya Mkoa wa Dodoma. Vipimo vya madaktari vinaonyesha alikuwa na malaria kali iliyoambatana na maumivu ya tumbo kiasi cha kusababisha ashindwe kula kwa muda mrefu. NATOA SHUKRANI ZANGU KWENU nyote mlionisaidia kwa namna yoyote ile katika kufanikisha safari yangu toka Arusha hadi Dodoma kuhudhuria mazishi. Tulimzika Jumamosi June 9, 2012 katika makaburi ya Msalato Mnadani. MUNGU AWABARIKI SANA.

Hapa pia ABRAHAM JOHN MLAULEanaonekana kushoto alipohudhuria "Send-Off" ya mtoto wa dada yetu mwaka jana. Amefariki akiwa na miaka 60 kamili, alizaliwa February 15, 1952.

Mwili wa ABRAHAM JOHN MLAULE ukifanyiwa sala katika Kanisa la St. John Msalato Anglican Parish

Dada yetu mkubwa Mrs. Sillah akimkabidhi  mtoto mkubwa wa marehemu aitwaye JOHN  majukumu ya kuwalea mama yake na wadogo zake. Alikabidhiwa "Biblia" iwe taa ya miguu yake katika uongozi huo, maana bila msaada wa Mungu hawezi kitu.

No comments: