TANESCO Mpya Iweje
Wapendwa
wateja wa TANESCO na wananchi wote kwa ujumla, Shirika la Umeme
Tanzania TANESCO ni mali ya Umma kwa kuwa linamilikiwa na Serikali kwa
asilimia 100. Hivyo TANESCO ni mali ya watanzania.
Kwa
kulitambua hilo, Uongozi wa Shirika umeanzisha mchakato wa kufanya
mabadiliko ya KIMUUNDO na KIUTENDAJI kwa Shirika, ili kuhakikisha kuwa
TANESCO inatoa huduma zake kwa ufanisi zaidi na kwa matakwa ya wananchi
na wateja wake.
Tunakaribisha
maoni, ushauri, mapendekezo kutoka kwa wananchi, wateja wote wenye
mapenzi mema na maendeleo ya TANESCO na nchi yetu kwa ujumla.
Tafadhali tutambue kuwa nia ya mchakato huu ni kujenga, hivyo tutoe maoni kwa nia njema.
Unaweza pia kutoa maoni yako kwa kupitia tanesco.iweje@tanesco.co.tz,
communications.manager@tanesco.co.tz au facebook kwa kutafuta neno
‘tanesco iweje’au kwa kupiga simu namba +255222451185
IMETOLEWA NA OFISI YA UHUSIANO,
TANESCO MAKAO MAKUU.
No comments:
Post a Comment