Thursday, December 13, 2012



Ni watu wengi wamehitaji kufahamu kuhusu kauli ya familia ya Marehemu mwigizaji/msanii Sharo Milionea baada ya tangazo la Airtel lenye sauti yake kuendelea kutumiwa na kampuni hiyo wiki kadhaa baada ya Sharo kufariki kwa ajali ya gari iliyotokea novemba 26 2012 Tanga.
Mjomba wa Marehemu ambae ndio msemaji wa familia Shaban Mkiete amethibitisha kwamba wamezungumza na kukubaliana na kampuni ya Airtel na hapa namkariri akisema “ni kweli tumekubaliana, kwa mujibu wa makataba wao lilikua linaisha terehe 31 mwezi huu tumekubaliana kwamba liendelee kwa makubaliano ambayo tumekubaliana nayo sisi kati ya mzee Majuto ambae bado yupo na familia ya Marehemu, mama mzazi wa Sharo Milionea ameridhia hilo hakuna tatizo”
Siku ya msiba millardayo.com ilipopata nafasi ya kuongea na mwakilishi wa Airtel alisema Marehemu Sharo Milionea alifariki ndani ya kipindi cha miezi 6 tu toka asaini dili la kuwa balozi wa Airtel na kufanya matangazo mbalimbali yeye na mzee Majuto.

Mama mzazi wa Marehemu.
Sio tu dili la Airtel, imefahamika tayari Sharo Milionea alikua amesaini mikataba mizuri na makampuni mbalimbali wakiwemo Wamarekani waliotengeneza filamu maarufu Afrika kama Yellow Card, Neria na nyingine ambapo kwa sasa Wamarekani hao wako hapa Tanzania na wametengeneza series kadhaa ikiwemo Wahapahapa na Siri ya Mtungi ambayo ndio Sharo Milionea kashiriki ndani na mpaka anafariki tayari alikua ameshaanza kucheza igizo hilo.
Unaweza kumsikiliza mjomba wa Marehemu akiongea hapo chini.

No comments: