Wednesday, January 16, 2013

Sheria ya kudhibiti umiliki wa bunduki New York

Majimbo kadhaa Marekani yanaruhusu umiliki wa bunduki
Jimbo la New York limeidhnisha sheria za kudhibiti matumizi ya bunduki Marekani. Mswaada huo unapunguza kiwango cha risasi na bunduki na kuanzisha kuchunguza afya za watu wanaotaka kununua bunduki.
Tangazo hilo limetolewa siku moja kabla ya Rais Barack Obama kutangaza mipango yake ya kudhibiti matumizi ya bunduki kitaifa.
Vile vile sheria hiyo inadhibiti ununuzi wa bunduki , ukubwa au udogo wa risasi ambazo mtu anaweza kununua hata kuifanya vigumu kwa mtu mwenye matatizo ya kiakili kununua bunduki.
Hii ndiyo sheria ya kwanza ya kudhibiti bunduki tangu mauaji ya kiholela ya watoto 26 na walimu katika eneo la Connecticut mwezi uliopita.
Jimbo la New York sasa lina sheria kali zaidi ya kudhibiti bunduki nchini Marekani.
Wabunge wa Democrats na wengi wa chama cha Republican waliunga mkono sheria hiyo ya kuruhusu tu risasi saba na kuongoza shughuli za kuwakagua watu wanaonunua silaha za kibinafsi.
Rais Obama anatarajiwa kuweka mikakati ya kudhibiti bunduki kitaifa

Kadhalika watu wanaotaka kununua bunduki wanachunguzwa akili yao kwanza.
Akitia saini mswada huo kuwa sheria Gavana wa New York Andrew Cuomo amesema ikiwa watu watatumia busara, mauaji ya kiholela ya bunduki yatakwisha.
Shirika la kitaifa linalotetea umiliki wa bunduki limesema kuwa sheria hiyo imepitwa na wakati.

No comments: