Aliyekuwa katibu mkuu wa chama tawla cha TANU enzi hizo Bw. Oscar Kambona akirejea nchini mwaka 1992 akiwa na binti yake, Neema, baada ya kuishi uhamishoni jijini London, Uingereza, kwa takriban miaka 25 kutokana na vuguvugu la kisiasa la wakati huo. Picha hii, aliyopiga Ankal uwanjani hapo, haikuwa rahisi kuipata. Wanahabari, waliofika hapo saa kumi alfajiri, walizuiwa kuingia ndani kwa ile hofu kwamba Bw Kambona angetiwa mbaroni na kutokea vuruguru. Ankal alipenya na kuwa wa kwanza kuipata taswira hii ambayo hadi sasa ndiyo iliyobaki kuonesha tukio hilo la kihistoria. Bw Kambona hakukamatwa na hakuna vurugu zilizotokea... |
This blog is for critical thinkers, people with open mind, ready to accept criticisms and work on them. Sharing the know-how, skills and experiences of Life and Technology at large. You are warmly welcome!! ---------------------------------------------------- Blogu hii ni kwa ajili ya wenye fikra makini wapendao kupokea na kufanyia kazi ukosoaji. Walio na mtazamo chanya tena mpana katika kushirikishana maarifa, ujuzi na uzoefu wa maisha na teknolojia kwa ujumla wake. Karibuni sana !!!
Friday, May 3, 2013
MIAKA ILE 1992 NA HOFU YA UPINZANI KULETA FUJO
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment