KIMENUKA BUNGENI; WABUNGE WAPIGA KELELE WAKITAKA MAJIBU KURA YA MAONI
SPIKA wa Bunge, Anne Makinda ameamua kulihairisha bunge hadi hapo
baadaye baada ya vurugu kuibuka kwa baadhi ya wabunge wakitaka hoja ya
kuhairisha mchakato wa kura ya maoni ijadiliwe na kura ya maoni isogezwe
mbele maana muda hautoshi.
Mbunge wa Ubungo (Chadema), John Mnyika alisimama na kusema:
"Nimesimama kupata idhini kwa mujibu wa kanuni ili shughuli za bunge
zisitishwe badala yake tujadili zoezi la uandikishaji nchi nzima mpaka
sasa zoezi halijakamilika hata kwa mkoa mmoja tu wa Njombe, jambo hili
ni la dharura na ilishatolewa na ukaagiza kamati ishughulikie, majibu
tupate kikao hiki na leo tunafunga mkutano hamna kitu"
Spika Makinda alijibu: Hoja hii inafanana na ile ya kwanza, nimesema majibu mtajibiwa baadae ndipo wabunge waliposimama na kupiga kelele wakitaka majibu na Spika Anne Makinda akalazimika kusitisha bunge hilo kwa muda.
Spika Makinda alijibu: Hoja hii inafanana na ile ya kwanza, nimesema majibu mtajibiwa baadae ndipo wabunge waliposimama na kupiga kelele wakitaka majibu na Spika Anne Makinda akalazimika kusitisha bunge hilo kwa muda.
===========================================================
MWANDISHI WA UJERUMANI ALIFAGILIA GAZETI LA ‘UWAZI’
Meneja
Mkuu wa Global Publishers, Abdalah Mrisho (kushoto), akiongea na
mwandishi Hawa Bihoga wa Idhaa ya Kiswahili Ujerumani (DW) ofisini kwake
Sinza-Bamaga jijini Dar es Salaam. Bihoga alifika hapo kulipongeza
gazeti la Uwazi na mwandishi Haruni Sanchawa. Mrisho akiagana na Bihoga.
MWANDISHI wa Shirika la Habari Idhaa ya Kiswahili Ujerumani (DW),
Hawa Bihoga, ametoa pongezi kubwa kwa kampuni ya Global inayochapisha
magazeti ya Championi , Ijumaa, Amani, Ijumaa Wikienda , Risasi na
Uwazi kwa kuibua matukio ya kipeke yanayosikitisha jamii kama lile
lililoandikwa kuhusu watoto watatu wakubwa wagonjwa wa akili waliofungiwa ndani na mama yao kwa miaka kumi.Bihoga alimpongeza mwandishi na Global Publishers, Haruni Sanchawa, kwa kufika katika eneo hilo na kufanikisha habari hiyo kufika gazetini. Aliongeza kwamba juhudi hizo ziliiwezesha serikali kujionea hali halisi ambayo baadhi ya jamii huishi katika mazingira magumu.
Mwandishi huyo wa Ujerumani pamoja na kuonana na mwandishi huyo alipokuwa katika ofisi za Global, alifanya pia mazungumzo na Meneja Mkuu wa kampuni, Abdalah Mrisho, ambapo alimpongeza kwa mipango bora ya kampuni kwa jumla.
Naye Mrisho alisema kampuni ilikuwa imefarijika sana kutokana na kupatikana kwa habari hiyo akisisitiza kwamba gazeti la Uwazi siku zote limekuwa likibua mambo mazito kama hayo.
Aliahidi kwamba habari nyingine nyingi kama hizo zitaendelea kufuatiliwa kwa gharama yoyote ili kuisaidia jamii ambayo inaishi katika mazingira kama hayo.
===========================================================
JENERALI MUHAMMAD BUHARI: RAIS MPYA NIGERIA
Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi
nchini Nigeria, INEC, Attahiru Jega amemtangaza rasmi Kiongozi wa wa
chama cha upinzani cha Nigeria Jenerali Muhammadu Buhari kuwa rais wa
taifa hilo kubwa barani Afrika baada ya kumbwaga rais wa zamani Goodluck
Jonathan.
===========================================================
WAZIRI LUKUVI AHITIMISHA ZIARA YA SIKU MBILI ASHUHUDIA UTENDAJI WA NHC
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Vangimembe
Lukuvi akikagua mradi wa nyumba za gharama nafuu za makazi za Kibada,
Kigamboni alipokuwa akikagua mradi huo jana mchana.
Nyumba za gharama nafuu za NHC Mwongozo, Kigamboni Dar es Salaam zinavyoonekana wakati Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Vangimembe Lukuvi alipozitembelea.
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi…
Nyumba za gharama nafuu za NHC Mwongozo, Kigamboni Dar es Salaam zinavyoonekana wakati Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Vangimembe Lukuvi alipozitembelea.
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi…
===========================================================
ASKOFU GWAJIMA ATOLEWA POLISI KWA DHAMANA
Askofu
wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima akiwa kwenye baiskeli ya
wagonjwa Hospitali ya TMJ Dar es Salam jana mchana akielekea Kituo cha
Polisi cha Oyterbay kupewa dhamana.
Gwajima akiingia kwenye gari huku akiwa na maumivu makali wakati akielekea kituoni hapo kupewa dhamana.
Wanahabari wakitoka kituo cha polisi Oysterbay kufuatilia …
No comments:
Post a Comment