
Na Musa Mateja wa GPL
Mwanadada anayetisha kunako tasnia ya filmu Bongo, Shamsa Ford (pICHANI jUU)ametoa kali baada ya kuweka wazi kuwa katika maisha yake hajawahi kulala na mwanaume katika nyumba ya kulala wageni ‘gesti’, Amani haliachi kitu.
Shamsa ambaye ametunuku penzi lake kwa jamaa mmoja aliyetajwa kwa jina moja la Dick wa Mikocheni Dar na kumwacha njia panda mchumba wake mjamaika, aliyasema hayo alipokuwa akigonga ‘spesho intavyu’ na Amani ndani ya Bilicanas Club, Posta, Dar mwishoni mwa wiki iliyopita.
“Huwezi amini, katika safari yangu ya mapenzi sijawahi kulala gesti na mwanaume, mara nyingi jamaa niliowahi ‘kutoka’ nao walikuwa wakinimpeleka kwenye ‘mageto’ yao,” alisema Shamsa.
Shamsa aliendelea kutambaa na mistari kwa kudai kwamba, amekuwa akijitahidi kumshawishi mwanaume anayemtaka kwenda naye sehemu yoyote kuvunja amri ya sita kwa sharti moja tu, siyo gesti.
Alisema: “Katika vitu ninavyochukia ni pamoja na kuona mtu akinishauri kuminya naye gesti.”
No comments:
Post a Comment