This blog is for critical thinkers, people with open mind, ready to accept criticisms and work on them. Sharing the know-how, skills and experiences of Life and Technology at large. You are warmly welcome!! ---------------------------------------------------- Blogu hii ni kwa ajili ya wenye fikra makini wapendao kupokea na kufanyia kazi ukosoaji. Walio na mtazamo chanya tena mpana katika kushirikishana maarifa, ujuzi na uzoefu wa maisha na teknolojia kwa ujumla wake. Karibuni sana !!!
Friday, November 14, 2008
Vipindi vya enzi hizo vya RTD unavikumbuka?
Wadau leo nimeona nije na hii nyingine, nimekumbuka sana ile miaka ya nyuma kidogo wakati tulikuwa hatuna radio stations nyingi kama zilivyo sasa, wakati huo station ilikuwa ni Radio Tanzania tu na ile idhaa yake ya kiingereza (External).
Fashion ya radio ilikuwa ni zile wanaita RADIO MKULIMA na brand names zake zilikuwa ni NATIONAL Panasonic ama PHILIPS. Mzazi alikuwa anainunua RTC (yale maduka ya uma).Tukirudi katika vipindi, navikumbuka sana vipindi vifuatavyo ambavyo bila shaka mdau utakubaliana na mimi vilikuwa maarufu kutokana na zile nyimbo za utangulizi kuashiria kipindi kuanza ama kumalizika.
"Sikiliza Bwana Umeme... (Bwana Umeme) - Kile kipindi cha TANESCO cha kuelimisha umma kuhusu matumizi mazuri ya umeme.
"Starehe na BP " - Uncle J. (Julius Nyaisanga) alikuwa anakimudu vyema kabisa""Kahawa ni Mali" - Namkumbuka sana yule mama wa kiashirio cha kipindi akitamka hayo maneno kwa rafudhi ya kichaga.
"Jifunze Kiswahili Fasaha" - sina uhakika kama nimeandika vyema tittle yake lakini kilikuwa ni kile kipindi kizuri kilichobuniwa kuhamasisha watu kuzungumza kiswahili katika harakati ya kuwaunganisha watu wa mikoani na wa Bara. Nakumbuka kiashirio chake kuna sehemu inasema.. na mikoani... ni kiswahili chatumika.....Bila kusahau vipindi kama..
"TTCL Simu kwa Maendeleo" kipindi cha "Serikali za Mitaa", " Afya yako /Afya ya jamii " sikumbuki vyema title ila nakumbuka kiashiria cha kipindi ulikuwa ni wimbo mmoja anaimba Kept John Komba na kundi lake wakati ule.
Ukija vipindi vya week ends kama "Club Raha leo Show", bila kusahau kipindi cha "Mama na Mwana" namkumbuka mtangazaji Edda Sanga alikuwa anakimudu vyema kipindi na zile hadithi za "Adili na Nduguze", "Kisa cha Mfalme Juha", ile hadithi ya watoto wa mfalme wanakwenda kutafuta wachumba wa kuoa... n.k wadau ongezeeni hapo kumbukumbu zenu.
Japokuwa kilikuwa ni kipindi cha watoto lakini nakumbuka watu wazima walikuwa wanazifuatilia kwa umakini sana zile hadithi bila kukosa sehemu hata moja juma moja baada ya lingine.
Wakati ule radio ilikuwa na msaada mkubwa kuelimisha jamii nzima (wakulima, wafanyakazi, wafanyabiashara) kuhusu mambo mbali mbali na watu walikuwa wanafuatilia sana.
Je, wewe mdau unakumbuka nini miaka hiyo hapo kunako Radio Tanzania (RTD)???
Fashion ya radio ilikuwa ni zile wanaita RADIO MKULIMA na brand names zake zilikuwa ni NATIONAL Panasonic ama PHILIPS. Mzazi alikuwa anainunua RTC (yale maduka ya uma).Tukirudi katika vipindi, navikumbuka sana vipindi vifuatavyo ambavyo bila shaka mdau utakubaliana na mimi vilikuwa maarufu kutokana na zile nyimbo za utangulizi kuashiria kipindi kuanza ama kumalizika.
"Sikiliza Bwana Umeme... (Bwana Umeme) - Kile kipindi cha TANESCO cha kuelimisha umma kuhusu matumizi mazuri ya umeme.
"Starehe na BP " - Uncle J. (Julius Nyaisanga) alikuwa anakimudu vyema kabisa""Kahawa ni Mali" - Namkumbuka sana yule mama wa kiashirio cha kipindi akitamka hayo maneno kwa rafudhi ya kichaga.
"Jifunze Kiswahili Fasaha" - sina uhakika kama nimeandika vyema tittle yake lakini kilikuwa ni kile kipindi kizuri kilichobuniwa kuhamasisha watu kuzungumza kiswahili katika harakati ya kuwaunganisha watu wa mikoani na wa Bara. Nakumbuka kiashirio chake kuna sehemu inasema.. na mikoani... ni kiswahili chatumika.....Bila kusahau vipindi kama..
"TTCL Simu kwa Maendeleo" kipindi cha "Serikali za Mitaa", " Afya yako /Afya ya jamii " sikumbuki vyema title ila nakumbuka kiashiria cha kipindi ulikuwa ni wimbo mmoja anaimba Kept John Komba na kundi lake wakati ule.
Ukija vipindi vya week ends kama "Club Raha leo Show", bila kusahau kipindi cha "Mama na Mwana" namkumbuka mtangazaji Edda Sanga alikuwa anakimudu vyema kipindi na zile hadithi za "Adili na Nduguze", "Kisa cha Mfalme Juha", ile hadithi ya watoto wa mfalme wanakwenda kutafuta wachumba wa kuoa... n.k wadau ongezeeni hapo kumbukumbu zenu.
Japokuwa kilikuwa ni kipindi cha watoto lakini nakumbuka watu wazima walikuwa wanazifuatilia kwa umakini sana zile hadithi bila kukosa sehemu hata moja juma moja baada ya lingine.
Wakati ule radio ilikuwa na msaada mkubwa kuelimisha jamii nzima (wakulima, wafanyakazi, wafanyabiashara) kuhusu mambo mbali mbali na watu walikuwa wanafuatilia sana.
Je, wewe mdau unakumbuka nini miaka hiyo hapo kunako Radio Tanzania (RTD)???
JK aongoza mazishi ya Richard Saidi Nyaulawa Mbeya
Rais Jakaya Mrisho Kikwete leo, Alhamisi, Novemba 13, 2008, amewaongoza mamia ya wananchi kumzika aliyekuwa Mbunge wa Mbeya Vijijini, Ndugu Richard Said Nyaulawa.
Mazishi hayo yamefanyika nyumbani kwa Mbunge huyo katika kijiji cha Inyala, kiasi cha kilomita 25 kutoka mjini Mbeya kwenye barabara kuu inayoekelea Iringa.
Rais Kikwete na mamia ya waombolezaji hao wameshuhudia mwili wa marehemu ukiteremshwa kaburini kiasi cha saa 9.20 mchana katika shamba lake kijijini hapo.
Mbali na Rais Kikwete, ambaye amefuatana na mke wake, Mama Salma Kikwete, mazishi hayo ya Ndugu Nyaulawa yamehudhuriwa na mawaziri, wabunge, wafanyabiashara, viongozi wa vyombo vya habari na mamia ya wananchi.
Rais Kikwete amewasili kwenye uwanja wa ndege wa mjini Mbeya kiasi cha saa nane mchana na kwenda moja kwa moja kijijini Inyala kwa ajili ya mazishi ya Mbunge huyo ambaye alifariki dunia usiku wa kuamkia Jumatatu ya wiki hii nyumbani kwake mjini Dar Es Salaam kwa ugonjwa wa kansa ya ini.
Kabla ya mwili wa marehemu kuteremshwa kaburini waombolezaji wameshuhudia salamu za rambirambi kutoka kwa viongozi mbali mbali akiwamo Mkurugenzi mwenza wa Kampuni ya Business Times Limited, Rashid Mbughuni, ambaye ameelezea ukaribu wa miaka mingi wa familia za akina Mbughuni na Nyaulawa.
Mbali na ubunge, Ndugu Nyaulawa alikuwa pia Mkurugenzi katika kampuni hiyo ya Business Times Limited.
Wengine waliozungumza kwenye mazishi hayo ni Mwenyekiti wa CCM wa Mkoa wa Mbeya, Ndugu Mullah; Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Ndugu John Mwakipesile; Naibu Spika wa Bunge, Ndugu Anna Makinda; Naibu Katibu Mkuu wa CCM, George Mkuchika; mwakilishi wa wabunge wa upinzani, Ndugu Mwadini Abbas Jecha, mwakilishi wa wabunge wa CCM, Dk. Mahenge.
Mara baada ya kukamilika kwa shughuli za mazishi hayo, Rais Kikwete ameondoka Mbeya kurejea Dar Es Salaam.
Mazishi hayo yamefanyika nyumbani kwa Mbunge huyo katika kijiji cha Inyala, kiasi cha kilomita 25 kutoka mjini Mbeya kwenye barabara kuu inayoekelea Iringa.
Rais Kikwete na mamia ya waombolezaji hao wameshuhudia mwili wa marehemu ukiteremshwa kaburini kiasi cha saa 9.20 mchana katika shamba lake kijijini hapo.
Mbali na Rais Kikwete, ambaye amefuatana na mke wake, Mama Salma Kikwete, mazishi hayo ya Ndugu Nyaulawa yamehudhuriwa na mawaziri, wabunge, wafanyabiashara, viongozi wa vyombo vya habari na mamia ya wananchi.
Rais Kikwete amewasili kwenye uwanja wa ndege wa mjini Mbeya kiasi cha saa nane mchana na kwenda moja kwa moja kijijini Inyala kwa ajili ya mazishi ya Mbunge huyo ambaye alifariki dunia usiku wa kuamkia Jumatatu ya wiki hii nyumbani kwake mjini Dar Es Salaam kwa ugonjwa wa kansa ya ini.
Kabla ya mwili wa marehemu kuteremshwa kaburini waombolezaji wameshuhudia salamu za rambirambi kutoka kwa viongozi mbali mbali akiwamo Mkurugenzi mwenza wa Kampuni ya Business Times Limited, Rashid Mbughuni, ambaye ameelezea ukaribu wa miaka mingi wa familia za akina Mbughuni na Nyaulawa.
Mbali na ubunge, Ndugu Nyaulawa alikuwa pia Mkurugenzi katika kampuni hiyo ya Business Times Limited.
Wengine waliozungumza kwenye mazishi hayo ni Mwenyekiti wa CCM wa Mkoa wa Mbeya, Ndugu Mullah; Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Ndugu John Mwakipesile; Naibu Spika wa Bunge, Ndugu Anna Makinda; Naibu Katibu Mkuu wa CCM, George Mkuchika; mwakilishi wa wabunge wa upinzani, Ndugu Mwadini Abbas Jecha, mwakilishi wa wabunge wa CCM, Dk. Mahenge.
Mara baada ya kukamilika kwa shughuli za mazishi hayo, Rais Kikwete ameondoka Mbeya kurejea Dar Es Salaam.
Subscribe to:
Posts (Atom)