This blog is for critical thinkers, people with open mind, ready to accept criticisms and work on them. Sharing the know-how, skills and experiences of Life and Technology at large. You are warmly welcome!! ---------------------------------------------------- Blogu hii ni kwa ajili ya wenye fikra makini wapendao kupokea na kufanyia kazi ukosoaji. Walio na mtazamo chanya tena mpana katika kushirikishana maarifa, ujuzi na uzoefu wa maisha na teknolojia kwa ujumla wake. Karibuni sana !!!
Friday, August 14, 2009
Tuesday, August 11, 2009
Naibu Waziri Mwantumu Mahiza aomba uume wa mwalimu aliyemjaza mimba mwanafunzi usifanye kazi
Na Juddy Ngonyani, Sumbawanga-Gazeti la Mwananchi
NAIBU Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Mwantumu Mahiza amewataka wananchi wa kijiji cha Muze wilaya ya Sumbawanga mkoani Rukwa kumuombea dua mbaya aliyekuwa mwalimu wa shule ya sekondari Mazoka aliyempa mimba mwanafunzi wa kidato cha tatu katika shule hiyo.
Mahiza alisema taarifa ya shule ilimsikitisha na baadhi ya matatizo yaliyoainishwa yatashughulikiwa na serikali.
" Na hili la huyu bazazi, aliyemkatisha masomo mwanafunzi ni lazima tumuombee dua ili asisimame daima,uume wake uache kufanya kazi" alisema.
Alisema mwalimu ndiye kioo cha jamii, lakini mwalimu anapomkatisha masomo mwanafunzi ni lazima achukuliwe hatua kali za kisheria na kinidhamu na kwamba kwa vile alitoroka dua limfuate huko aliko.
Awali akitoa taarifa ya shule hiyo mkuu wa shule hiyo Anicent Mpemba alisema katika kipindi cha miaka mitatu hadi hivi sasa wanafunzi wanne wa kike walikatishwa masomo yao kutokana na ujauzito.
Hata hivyo wanaume watatu walikamatwa kwa tuhuma za kutunga mimba hizo, lakini mwanaume wa nne alitoroka.
Mpemba alisema mwalimu huyo baada ya kupatikana na hatia alifanikiwa kutoroka kabla ya kukamatwa na juhudi za kumtafuta bado zinaendelea kwa lengo la kumfikisha katika vyombo vya sheria
NAIBU Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Mwantumu Mahiza amewataka wananchi wa kijiji cha Muze wilaya ya Sumbawanga mkoani Rukwa kumuombea dua mbaya aliyekuwa mwalimu wa shule ya sekondari Mazoka aliyempa mimba mwanafunzi wa kidato cha tatu katika shule hiyo.
Mahiza alisema taarifa ya shule ilimsikitisha na baadhi ya matatizo yaliyoainishwa yatashughulikiwa na serikali.
" Na hili la huyu bazazi, aliyemkatisha masomo mwanafunzi ni lazima tumuombee dua ili asisimame daima,uume wake uache kufanya kazi" alisema.
Alisema mwalimu ndiye kioo cha jamii, lakini mwalimu anapomkatisha masomo mwanafunzi ni lazima achukuliwe hatua kali za kisheria na kinidhamu na kwamba kwa vile alitoroka dua limfuate huko aliko.
Awali akitoa taarifa ya shule hiyo mkuu wa shule hiyo Anicent Mpemba alisema katika kipindi cha miaka mitatu hadi hivi sasa wanafunzi wanne wa kike walikatishwa masomo yao kutokana na ujauzito.
Hata hivyo wanaume watatu walikamatwa kwa tuhuma za kutunga mimba hizo, lakini mwanaume wa nne alitoroka.
Mpemba alisema mwalimu huyo baada ya kupatikana na hatia alifanikiwa kutoroka kabla ya kukamatwa na juhudi za kumtafuta bado zinaendelea kwa lengo la kumfikisha katika vyombo vya sheria
Friday, August 7, 2009
mdau akipiga taswira ya banda la kuuzia gesi Kigamboni lililowaka moto na kutokea milipuko mikubwa asubuhi ya leo. mtu mmoja amejeruhiwa na nyumba kama tano hivi zimeharibika kutokana na mripuko huo ulioleta fadhaa kwa wakazi wa kigamboni na katikati ya jiji ambako milio ilisikika kama mabomu ya mbagala
KWA HISANI YA MICHUZI BLOG: http://issamichuzi.blogspot.com
Thursday, August 6, 2009
Tuesday, August 4, 2009
Subscribe to:
Posts (Atom)