Monday, June 11, 2012

STARS YAWASHA INDIKETA SAFARI YA BRAZIL 2014




Kikosi kilichofanya mauaji leo
Erasto Nyoni mfungaji wa bao la ushindi


Shomary Kapombe aliyesawazisha
Boban akisaidia ulinzi

Boban kabla ya kuingia kulia akiwa na Nurdin Bakari benchi

Boban kulia, Nurdin katikati na Shaabn Nditi



Dk Mwankemwa akimtibu jeraha Ngassa

Kaseja akiokoa moja ya hatari langoni Stars


Mwinyi Kazimoto akiwaongoza wenzake kutoka uwanjani baada ya mechi



TIMU ya soka ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars imeibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Gambia jioni hii kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, katika mechi ya pili ya Kundi C, kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Kombe la Dunia mwaka 2014 nchini Brazil.

Stars ilitoka nyuma kwa 1-0 kipindi cha kwanza na kuibuka na ushindi huo- kwa mabao ya kipindi cha pili ya Shomari Kapombe dakika ya 60 na Erasto Nyoni dakika ya 87 kwa penalti, baada ya beki mmoja wa Gambia kuunawa mpira kwenye eneo la hatari.
Stars ambayo mechi ya kwanza ilifungwa 2-0 na wenyeji Ivory Coast mjini Abidjan Jumamosi iliyopita, kipindi cha kwanza ilicheza ovyo kidogo, lakini kuingia kwa Haruna Moshi ‘Boban’ aliyechukua nafasi John Bocco ‘Adebayor’ kipindi cha pili, kuliifanya Tanzania icheze kwa uhai na kulitia misukosuko lango la Gambia hatimaye kupata mabao hayo mawili.
Gambia walitangulia kupata bao lililofungwa na Mamadou Ceesay dakika ya nne.
Stars sasa imejinasua mkiani mwa kundi C na kupanda nafasi ya pili badaaye Morocco kutoa sare ya 2-2 jana na Ivory Coast inayoongoza kwa pointi zake nne.
Kwa Stars huu ni ushindi wa kwanza nyumbani tangu waifunge Jamhuri ya Afrika ya Kati Machi 26, mwaka jana.



Vikosi vya Tanzania kushoto na Gambia kulia





Mfungaji wa bao la Gambia dakika ya nane, Mamadou Cesay akishangilia







Samatta anayetarajiwa kuongoza safu ya ushambuliaji Stars hapa akidhibitiwa na kolo Toure Jumamosi iliyopita Abidjan


TIMU ya soka ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars  inashuka kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, kumenyana na Gambia katika mechi ya pili ya Kundi C, kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Kombe la Dunia mwaka 2014 nchini Brazil.
Stars ambayo mechi ya kwanza ilifungwa 2-0 na wenyeji Ivory Coast mjini Abidjan Jumamosi iliyopita, itacheza mechi ya tatu chini ya kocha mpya, Kim Poulsen, aliyerithi mikoba ya Mdenmark mwenzake, Jan Poulsen.
Poulsen amekiri kucheza mechi mbili bila kufunga hata bao moja, sare ya bila kufungana na Malawi na kichapo cha 2-0 cha Ivory Coast, lakini amesema timu yake imebadilika mno na anatarajia mabao katika mchezo wa leo.
Poulsen amesikitishwa na kitendo cha Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), kushindwa kumpatia DVD za mechi za Gambia kuelekea mechi ya leo na jana alisema hiyo ni mara ya pili anaomba DVD, lakini anashindwa kupatiwa, baada ya awali kuomba DVD za Ivory Coast.
Pamoja na kukosa DVD hizo, lakini Poulsen amesema amewaandaa vizuri vijana wake kwa ajili ya mechi hiyo, ili washinde na kujiweka kwenye nafasi nzuri ya kuwania tiketi ya Brazil 2014.
Poulsen alisema kambi yake iko vizuri na anafurahi kiungo mshambuliaji Haruna Moshi Shaaban ‘Boban’ aliyekuwa mgonjwa kiasi cha kukosa safari ya Ivory Coast, anaendelea vizuri na anaweza akaanza leo.
Kwa upande wake, kocha wa Gambia, Mtaliano, Luciano Machini amesema mechi ya leo itakuwa ngumu kwa sababu wapinzani wao ni wazuri.
Machini aliyechukua nafasi ya aliyekuwa bosi wake, Peter Bonu Johnson, Mei mwaka huu, amesema kwamba Taifa Stars ni wazuri na wana kasi uwanjani, hivyo mechi hiyo hata wachezaji wake wanajua itakuwa ngumu.
Alisema wao walicheza vizuri dhidi ya Morocco kwenye mechi yao ya kwanza, lakini wanaingia kwenye mechi ngumu na wenyeji leo.
Nge wa Gambia waliotoka sare ya 1-1 nyumbani na Morocco kwenye mechi ya kwanza Jumamosi, wamecheza mechi nne bila kushinda, tangu washinde kwa mara ya mwisho Agosti 10, mwaka jana mabao 3-0 katika mchezo wa kirafiki dhidi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC).
Ilifungwa 1-0 na Namibia Septemba 3, mwaka jana, ikatoka sare ya 1-1 na Burkina Faso Oktoba 8, mwaka jana, ikafungwa 2-1 na Algeria Februari 29, mwaka huu kabla ya kutoka sare ya 1-1 na Morocco nyumbani Jumamosi iliyopita.
Rekodi ya Tanzania pia si nzuri katika mechi za nyumbani na tangu iifunge Jamhuri ya Afrika ya Kati Machi 26, mwaka jana haijashinda tena mechi kwenye Uwanja huo wenye uwezo wa kuchukua mashabiki 60,000 na imecheza saba baada ya hapo.
Katika mchezo wa leo, kikosi cha Stars kinatarajiwa kuwa; J. Kaseja, Kelvin Yondan, Amir Maftah, Juma Nyosso, K. Yondan, M. Ngassa, S. Nditi, M. Kazimoto, M. Samata, H. Moshi na S. Abubakar.
Gambia: C. Allen, A. Jammeh, O. Koli, M. Danso, T. Jaiteh, Y. Ceesay, P. Jagne,
P. Kujabi, M. Jarju D. Savage na M. Ceesay.


Kikosi cha Stars kilichoifunga Afrika ya Kati


MATOKEO YA STARS TAIFA TANGU ISHINDE MARA YA MWISHO:
Machi 26, 2011: Tanzania 2 – 1 Afrika ya Kati (Kufuzu CAN)
Mei 14, 2011: Tanzania 0 – 1 Afrika Kusini (Kirafiki)
Sept 3, 2011: Tanzania 1 – 1 Algeria (Kufuzu CAN)
Nov 15, 2011: Tanzania 0 – 1 Chad (Kufuzu Kombe la Dunia)
Des 3, 2011: Tanzania 1 – 2 Zimbabwe (Kirafiki)
Feb 23, 2012: Tanzania 0 – 0 DRC (Kirafiki)
Feb 29, 2012: Tanzania 1 – 1 Msumbiji (Kufuzu CAN)
Mei 26, 2012: Tanzania 0 – 0 Malawi (Kirafiki)

No comments: