Tuesday, July 24, 2012

RISASI ZACHAFUA ILALA NI BAINA YA ASKARI NA MAJAMBAZI WANNE

Mmoja wa askari akijaribu kuikoki unduki yake kwa ajili ya mpambano na majambazi waliokuwa  wamejificha ndani maeneo ya Ilala Sharf Shamba jijini Dar es Salaam.Tukio hili limetokea jana majira ya saa 7 na nusu mchana.
 Majibizano ya Risasi baina ya Polisi na Majambazi leo yameonekana wazi  katika wilaya ya Ilala mataa wa Sherf Shamba baada ya Majambazi sita waliokuwa wanajaribu kuwakimbia askari katika maeneo hayo.
Majambazi hao waliokuwa wanatupiana risasi na askari amabapo majibizano yalidumu kwa takriban saa mbili walitokea maeneo ya Barabara inayotoka Posta kuelekea Buguruni wakiwa na gari ndogo aina ya Saloon yenye namba za usajili T 169 AKM walikuwa wanafwata na Defender ya Polisi.
Baada ya majibizano hayo Majambazi waliishiwa nguvu baada ya kuishiwa risasi na hatimae Polisi wakawakamata wakiwa wane na wote wanaume.

Bunduki inasumbua kidogo na mwenzake anaangalia usalama , wakati huo Majambazi waliokuwa  wamejificha ndani katika nyumba iliyopo pembeni kidogo na askari hao.

Hapa Bunduki imekwama sasa anakwenda kubadilisha

Tayari ameipata nyingine kwahiyo ni kazi mwendo mmoja

Defender moja ya polisi iliyokuwemo maeneo hayo

Askari akiangalia usalama akiwa kwenye Gari lao

Askari walimwagika balaa na ilikuwa ni shughuli nzito

Hapa wanasubiri kama majambazi watasalimu Amri.

Hili gari limewahifadhi majambazi wawili ambao wanalindwa na askari baada ya kufanikiwa kuwakamata ikiwa bado kuna majambazi wengine ambao bado hawajatoka ndani na wanaendelea kupiga risasi juu .

 Moja ya Jambazi aliyekamatwa na askari hao na nyumba yenye geti jekundu ndimo ambapo  majambazi hao walikuwa wamejificha.

Hili ni gari ambalo majambazi hao walikuwa wanalitumia.

No comments: