Wednesday, December 5, 2012

NYATI AZAA BINADAMU

Bangkok Thailand
KATIKA hali ya kustaajabisha, nyati anayefugwa na raia mmoja anayeishi nje kidogo ya Jiji la Bangkok nchini Thailand amezaa kiumbe kinachofanana na binadamu kwa asilimia 80.
Mashuhuda walisema kiumbe hicho kilichozaliwa hivi karibuni, kuanzia kichwani kwenda hadi tumboni ni mwonekano wa kibinadamu.
Hata hivyo, miguu na mikono yake ina kwato kama za mama yake ambaye ni nyati lakini kichwani hakuna  pembe.
Tangu kusikika kwa tukio hilo, umati kutoka sehemu mbalimbali za jiji hilo umekuwa ukifika nyumbani kwa mfugaji huyo ambaye hakutajwa jina kwa lengo la kutaka kushuhudia ‘laivu’ tukio hilo la ajabu na hivyo kuzua taharuki.
“Kutokana na wingi wa watu kufurika, polisi waliitwa ili kuhakikisha kunakuwa na amani ya kudumu na watu walitawanywa huku wakisema mfugaji huyo ndiye pekee anayejua kilichosababisha mnyama huyo kuzaa kiumbe kinachofanana na binadamu,” alisema shuhuda mmoja. Taarifa zinasema, kiumbe hicho mara baada ya kuzaliwa hakikuchukua muda mrefu kikafa. Hili ni moja ya tukio la ajabu linalotajwa kutokea duniani.

No comments: