Nyoka hao wana uzito wa kilo 250 na mtu anayefanyiwa massage anaweza
kupiga kelele au hata kupumua bila nyoka hao kufanya chochote.
Unaweza
usifikirie kama kuna kitu kama hiki kinafanyika lakini mbuga hii
iliyopo katika mji wa Cebu nchini Ufilipino inapata wateja wengi sana
wakipanga foleni kusubiri huduma ya kukandwa mwili “Massage” ambayo
hutolewa bure lakini kwa wanaoweza tu kuhimili mikiki yake.
Nyoka hao wakubwa wanne waliopewa majina ya Michelle, Walter, EJ and
Daniel hutolewa nje kutoka kwenye eneo wanapofugwa na kuwekwa juu ya mtu
anayetaka huduma huyo wakati mtu huyo akiwa amelala chini kwenye
kitanda maalum karibu na lango kuu la kuingilia katika mbuga hiyo.
Watu wengi wanashangazwa na mbuga hii na huduma inayotolewa sasa jiulize unaweza kufanya hivyo hata kama una uchovu kiasi gani?
No comments:
Post a Comment