
Mkuu wa Majeshi nchini Jenerali Davis Mwamunyange pichani akizungumza na baadhi ya vyombo vya habari,alisema kutimiza miaka 46 kwa Jeshi hilo kumeendana na maboresho mbalimbali yenye lengo la kuleta tija katika katika suala zima la ulinzi wa amani mipaka ya nchi.
Pamoja na hayo Jenerali Mwamunyange aliongeza kuwa kwa muda wa karibuni Jeshi la Tanzania limekuwa likifanya maonesho mbalimbali yanayosaidia kuonesha wananchi masuala yanayohusu Jeshi lao.
Akielezea historia ya Jeshi hilo Jenerali Mwamunyange alisema kuwa awali maadhimisho hayo yalifanyika baada ya miaka 10 ambapo kwa sasa yanafanyika kila baada ya miaka 5 yenye kushirikisha Jeshi lote nchini.
Kila mwaka JWTZ huadhimisha wiki ya majeshi ambapo kwa kawaida huanza tarehe 26/8/2010 hadi tarehe 1/9/2010 ambapo mwaka huu sherehe hizo ziliadhimishwa katika kambi ya wanajeshi wa majini kituo cha kigamboni ambapo mgeni rasmi alikuwa Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Dokta Hussein Mwinyi.
No comments:
Post a Comment