This blog is for critical thinkers, people with open mind, ready to accept criticisms and work on them. Sharing the know-how, skills and experiences of Life and Technology at large. You are warmly welcome!! ---------------------------------------------------- Blogu hii ni kwa ajili ya wenye fikra makini wapendao kupokea na kufanyia kazi ukosoaji. Walio na mtazamo chanya tena mpana katika kushirikishana maarifa, ujuzi na uzoefu wa maisha na teknolojia kwa ujumla wake. Karibuni sana !!!
Tuesday, January 31, 2012
Picha mbalimbali za Harrison Mwakyembe, Samuel Sita na James Lembeli
![]() |
| Kumbuka ameugua sana ugonjwa wa ngozi, ona amevaa kofia na glovu kuhifadhi mwili. Samwel Sita anasema kalishwa sumu. Du mi simo aisee wanajua wenyewe. Ila inasikitisha sana. |
![]() |
| Samwel Sita madhabahuni kanisa la Ufufuo na Uzima kwa Mchungaji Gwajima Kawe Dar es Salaam |
![]() |
| Walio katika mapambano na ufisadi, kushoto kwenda kulia ni Anne Kilango, Samwel Sita, James Lembeli na Harrison Mwakyembe. |
![]() |
| Hapa Mwakyembe anaonekana kwa karibu, kulia kwake ni James Lembeli |
![]() |
| Samwel Sita akishuka ngazi |
Baridi kali yauwa watu 36 Ulaya mashariki
![]() |
| Msichana akichungulia nje ya dirisha baada ya kuweka mkono kufuta barafu huko Ukraine Ulaya mashariki |
Monday, January 30, 2012
Waliopigana vita Iraq wakaribishwa Marekani
![]() |
| Washiriki wa gwaride/maandamano ya heshima ya kuwapokea/kuwakumbuka waliopigana vita vya Iraq. Sherehe hio ilifanyika huko ST. Louis Marekani, wapo waliouawa na wapo waliorudi salama. |
Watu 26 wauawa katika tukio la moto nchini Peru.
![]() |
| Baadhi ya ndugu wa watu waliokumbwa na tukio hilo wakifuatilia kwa majonzi zoezi la uokoaji. Ni huzuni kwa kweli |
Friday, January 27, 2012
Usitawale nchi ukajisahau, huyu yamemkuta
Dikteta wa zamani wa nchi ya Guatemala Efrain Rios Montt afikishwa mahakamani kwa mauaji ya kimbali aliyofanya wakati akitawala nchi hiyo
![]() |
| Diktetea huyo akiwa mesimama katikati ya askari wa usalama wakati wa usikilizaji wa kesi yake jana Alhamisi Januari 26, 2012 |
![]() |
| Baadhi ya ndugu wa watu walioawa wakati wa utawala wa dikteta huyo, wakisikiliza kesi hiyo |
![]() |
| Bango kubwa lenye baadhi ya picha za watu waliopotea na yaaminika waliuawa na dikteta huyo Efrain Rios Montt |
Novak Djokovic amchapa Andy Murray katika nusu fainali-Tennis
Alimpa kichapo cha 6-3, 3-6, 6-7, 6-1, 7-5 katika mashindano ya Australian Open. Ona alivyolala kwa furaha.
![]() |
| Hapa akimpongeza kwa kushindana naye (Andy Murray ni huyo kulia) |
![]() |
| Novak akirudisha mpira |
![]() |
| Andy akishangilia kushinda seti ya 3, lakini mambo yalimgeuka baadae |
![]() |
| Hapa ndio shughuli nzima ilipofanyika |
Wajishona midomo na kujikata mwilini, akina nani na kwanini?
![]() |
| Angalia huyu alivyojikata mikononi, ni ujasiri haswa ila hauna maana kwavile anajiumiza mwenye, je akifa hiyo hali nzuri gerezani itamsaidia nini? |
![]() |
| Ilibidi askari wa gereza watembelee vyumbani kuna hali halisi. Duniani kuna mambo. Kuishi kwingi kuona mengi. |
Thursday, January 26, 2012
Mabadiliko makubwa Facebook, kuwa makini
Facebook ikiwa ni nyumba ya online kwa mamilioni ya watu duniani, hivyo mabadiriko yanayotokea kwenye facebook ni dhahiri yanaathiri kwengi wetu. Katika siku za karibuni Facebook wamekuja na kitu kipya mbacho wenyewe wanakiita Timeline , hii Timeline ni mpangilio mpya wa kurasa ya facebook ambao unamuwezesha mtumiaji kupanga picha,matukio nk kulingana na muda husika.

Picha inayoonesha muonekano wa timeline ndani ya Facebook.
Katika Timeline, utaweza kupanga taarifa zako kwa mtindo wa kipekee zaidi huku ikimpa nafasi mtembeleaji kuzipitia kwa haraka zaidi. Kama utaangalia picha ya hapo juu, utaona kwenye timeline yangu mtu akija mara ya kwanza ataona marafiki,picha na mengine meengi. Siyo hayo tu, kwa kutumia timeline mtu anaweza kuangalia matukio yako toka siku ya kwanza uliyojiunga na facebook.
Katika siku zilizopita Timeline ilikuwa ni kwa wanaohitaji, ila kuanzia tarehe moja mwezi wa pili timeline itakuwa ni lazima, utake usitake ni lazima utumie au kwa lugha ya kiufundi tunaweza iita de

fault. Hivyo usishangae kuona mabadiriko kwenye kurasa yako.
Kitu ambacho kimenivuta kuandika hii makala ni kuwa, ingawa timeline ni nzuri na ya kuvutia, ila Facebook inaonekana wanazidi kufanya mambo kuwa magumu,nidhahiri kuwa kufanikiwa kwa facebook kumekuja kutokana na urahisi wa utumiaji. Hivyo kufanya mambo kuwa magumu kutawafanya watu wengi kuikimbia au kushindwa kuifungua hususan wale walio kwenye mgao wa bandwith (internet zilizo taratibu mno). Kuna siku niliwahi kuona mpachiko wa rafiki yangu ambaye ni mtumiaji mzuri mno wa faceboo, yeye alikuwa akilalamika kwa kusema nani amesema tunataka hii timeline?
Kitu kingine kikubwa ambacho kinaniumiza kichwa ni privacy, facebook wenyewe mara kibao wamekiri kuwa privacy ni moja ya vitu vinavyowaumiza kichwa, kwenye facebook ya sasa mtu anaweza kuona matukio yako ndani ya wiki hadi mwezi,ila sasa kwenye hii timeline mtu anaona tukio tangu siku ya kwanza uliojiunga facebook, sasa huku si kuwaumbua watu? Chukulia mfano kwa wale wenzangu na mimi wazee wa kuongopa, huu si ndio mwanzo wa kukamatwa? Hivyo basi kwa kuweka timeline kuwa default kutawatatiza wengi. Habari njema ni kuwa kuanzia sasa unaweza kuanza kufuta matukio kadhaa usiyopenda kuwaonesha watu hadi hapo januari 31.
Je wewe unalionaje hili?
Bomu walilolengwa askari wa NATO lawauwa waAfghanstan 4
![]() |
| Gari lenyewe lililolipukiwa na bomu ndio hili hapa eneo la tukio |
Je mjadala wa VAZI LA TAIFA ni muhimu kwa waTanzania muda huu?


Kwa nini tunashindwa kuelewa ukweli huo mdogo ambao hata watoto wa shule za msingi wanaufahamu?
Kuna wakati wapenda muziki walikaa na kuamua eti mtindo wa dansi nchini uitwe “Achimenengule”! Kilichofuata ni kwamba uamuzi huo uliishia kwenye meza walizokuwa wamezikalia wakati wa majadiliano hayo.
Hapakuwa na “Achimenengule” wala nini hadi leo!
Mtindo wa mavazi au kitu chochote huwa havipangwi, hujitokeza vyenyewe kwa kukubalika kimyakimya kwa watu – si kwa kutangazwa!
Hivi hatuna kitu cha maana cha kujadili kwa manufaa ya watu wengi? Kwa nini Wizara ya Habari, Michezo na Utamaduni inakubali kujishusha kiasi hicho wakati majuzi tu ilishindwa kuisafirisha timu ya wanawake ya taifa ya soka kwenda Namibia wakati kila mwaka inapewa bajeti nono na bunge?
Iwapo tatizo ni Watanzania kutaka kujulikana nje ya nchi, basi dawa yake ni ndogo sana. Mtanzania anayetaka kujulikana akiwa nje ya nchi hii ni kuvaa nguo yoyote na akaiandika kwa maandishi makubwa sehemu yoyote, kwa mfano: “I am a Tanzanian” (kwa Kiingereza), “Je suis un Tanzanien” (Kifaransa) au “Yo soy on tanzano” (Kihispania).
Yote hayo yanamaanisha kwamba: “Mimi ni Mtanzania”.
Hiyo inatosha kabisa kuwafanya watu wakufahamu kwamba unatoka katika nchi mojawapo za bara maskini la Afrika. Inatosha!
Huna haja ya kuchora picha ya twiga au mlima Kilimanjaro kwani twiga ni wengi sana duniani achilia mbali milima mirefu zaidi ya Kilimanjaro.
Hata hivyo, kwa kifupi kabisa: Watu waliopania kwamba Tanzania lazima iwe na vazi la taifa ambalo litawatambulisha wakiwa ndani na nje ya nchi hii, wasipoteze muda kulitafuta – watumie mavazi ya Kimasai!
Ni mavazi yenye kuvutia na ni ya kipekee ambayo Mtanzania akivaa nje ya nchi hii ni hakika watu watamshangaa na kumfurahia.
Kama vazi hili watu hawalitaki basi ni heri tujadili jinsi ya kuzipatia shule za sekondari za kata kompyuta, tujadili jinsi ya kusomesha na kuwalinda maalbino nchini, tujadili jinsi ya kupunguza bei za betri za radio ili mamilioni ya maskini nchini waweze kuzitumia kirahisi kwa radio na tochi zao.
Kujadili mashati na magauni ya kuvaa wakati tuko kwenye ndege tukielekea Ulaya au wakati tuko kwenye semina za kujadili posho ni kupoteza wakati na raslimali za taifa bure.
Hivi Watanzania hatuna cha maana cha kufanya kwa ajili yetu na wajukuu zetu?
Usipoamini shauri yako! Huyo mama sio mtu ni SANAMU
![]() |
| Huyu nae ameamua kusogelea kwa karibu sana lakini haibadiliki kuwa mtu BADO INABAKI KUWA SANAMU TU. |
Polisi wa Colombia wateketeza mitambo ya Mihadarati
![]() |
| Helikopta mbili (Hii ya karibu na ile ya mbali) zikiruka juu ya anga la Puerto Concordia wakati wa zoezi hilo |
![]() |
| Askari wa kikosi maalum cha kupambana na dawa za kulevya wakikagua mitambo haramu ya kutengenezea dawa hizo huko Puerto Concordia, Colombia |
Kasheshe nzito apata Waziri Mkuu wa Australia
![]() |
| Mlinzi wake akijitahidi kumwepusha na hatari ya wavamizi hao wa Aboriginal. Kwanza alijificha ndani ya jengo kwa takriban dakika 20, kisha ndio ukafanyika mpango wa kumtorosha. |
Tuesday, January 24, 2012
Soma habari hii, utashangaa sana!!
Subscribe to:
Posts (Atom)













































